Dini ya Uislamu

Inatangazwa kupitia Dalili zitokanazo na Qur'ani na Sunnah za Mbora wa Viumbe.

Muhammadi ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu

Kuamini ujumbe wa Mtume Muhammad- rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- ndiye upande wa pili wa nguzo za msingi katika nguzo za uislamu, na msingi mkuu ambao jengo lake husimama juu yake.

Na mtu huwa muislamu kwa baada ya kutamka shahada mbili, hivyo atashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake, na atashuhudia kuwa Muhammadi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

B- Basi ni nini maana ya Mtume? na ni nani huyo Muhammadi? na je kuna Mitume wengine wasiokuwa yeye?

Swali hili ndilo tutakalojaribu kulijibu katika kurasa hizi.

Mtume ni mtu aliye katika kilele cha juu kutokana ukweli wa maneno na tabia njema Mwenyezi Mungu anamchagua katika watu na humfunulia wahyi kwa akitakacho katika mambo ya dini na mambo yaliyofichikana na anaamrishwa kuwafikishia watu, hivyo Mtume ni mwanadamu, na mfano wake ni kama binadamu wengine, anakula kama wanavyo kula, na anakunywa kama wanavyokunywa, na anahitajia kila anachokihitajia mwanadamu, lakini yeye anatofautiana nao kwa kupewa wahyi ambao unamjia toka kwa Mwenyezi Mungu na akamuonyesha yatakayotokea katika mambo yaliyofichikana, na mambo ya dini ambayo anayafikisha kwa watu, na anatofautiana nao vile vile kwa yeye kuwa na ulinzi wa Mwenyezi Mungu unaomzuia kutenda madhambi makubwa na kila jambo ambalo linaharibu ufikishaji wa ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa watu.

Na tutaleta mfululizo wa baadhi ya visa vya Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammadi -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- ili iwe wazi kwetu kuwa ujumbe wa Mitume ni mmoja nao ni kulingania katika kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake, na tunaanza kuleta kisa cha mwanzo wa kuumbwa Mwanadamu na uadui wa Shetani kwa Baba wa wanadamu na kizazi chake.

About The Author

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *